Adbox

Wednesday, November 27, 2019

Abiria wanusurika kifo baada ya kupewa Biskuti zinazodhaniwa kuwa na dawa za kulevya

Abiria wawili waliokuwa wanasafiri na basi la kampuni ya Buti la Zungu kutoka Dar es Salaam kuelekea mkoani Mtwara wamenusurika kifo baada ya kupewa Biskuti zinazodhaniwa kuwa na dawa za kulevya na watu waliokaa nao na kuibiwa.

Waliokumbwa na mkasa huo ni Dadi Mohamedi (49) na Omary Burian (27), wote wawili wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Lindi 'Sokoine' kwa matibabu zaidi.

Tayari Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi amesema anazo taarifa na wanaendelea na taratibu za Kipolisi kisha baadae atatoa taarifa zaidi.

No comments:

Post a Comment

Adbox