Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika jitihada za kuboresha huduma ya Afya linatarajia kuzindua Idara mpya ya huduma ya Tiba ya Dialysis katika Hospitali Kuu ya Jeshi, Lugalo.
Shughuli za uzinduzi huo zinatarajia kufanyika kesho Jumatano tarehe 23 Oktoba, 2019 kwenye Hospitali kuu ya Jeshi Lugalo iliyopo Jijini Dar es Salaam kuanzia saa mbili na nusu (2:30) asubuhi.
Mgeni rasmi katika shughuli hiyo anatarajiwa kuwa Waziri wa Ulinzi na JKT, Dkt. Hussein Ali Mwinyi.
JWTZ limealika vyombo vya Habari kwenye hafla hiyo muhimu ili kuuhabarisha umma juu ya huduma hiyo kupatikana Jeshini.
Tuesday, October 22, 2019
Taarifa kuhusu uzinduzi wa huduma ya tiba ya Dialysis Hospitali Kuu ya Jeshi
Tags
# Top News
About Sultan Mapigo
SULTAN MAPIGO: Kuwa wa kwanza kuhabarika, Tafadhari usisahau kusubscribe kushare na kucomment
Top News
Tags:
Top News
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment