Bondia Hassan Mwakinyo jana amepokea cheti cha pongezi toka kwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa aliyemuwakilisha Waziri Mkuu katika kongamano la Mzalendo Jasiri linalomalizika leo katika ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Center.
Mwakinyo amepatiwa cheti hicho kwa kuwa kijana mwenye ushawishi katika jamii na anayefanya vizuri kimichezo katika medani za kimataifa akiiwakilisha vyema Tanzania.
Bondia Mwakinyo anatarajiwa kupanda ulingoni Novemba 29 mwaka huu kupigana na Arnel Tinampey toka nchini Philippines ikiwa ni pambano lake la Kwanza la kimataifa kufanyikia nchini Tanzania.
Saturday, October 19, 2019
Bondia Hassan Mwakinyo apokea cheti cha pongezi
Tags
# Top News
About Sultan Mapigo
SULTAN MAPIGO: Kuwa wa kwanza kuhabarika, Tafadhari usisahau kusubscribe kushare na kucomment
Top News
Tags:
Top News
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment