Na. John Walter-Babati-Manyara
Askofu Msaidizi wa Jimbo kuu katoliki la Arusha Mhashamu Prosper Lymo amewataka Mashemasi wannne waliopata daraja hilo takatifu kutumia vipawa walivyo navyo katika kujitolea kumtumikia mungu.
Wito huo ameutoa katika Misa takatifu ya kuwapatia daraja ya ushemasi mashemasi hao, iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Yosefu Parokia ya Magugu jimbo katoliki la Mbulu.
Mhashamu Baba Askofu amewasisitiza watii wito huo kwa kuwahubiria watu Injili kama alivyokuwa akiifundisha Bwana Yesu Kristu.
Misa hiyo Takatifu imehudhuriwa na waamini,viongozi wa kanisa Katoliki wakiwemo watawa wa mashirika mbalimbali ,mapadre wa jimbo la Mbulu,pamoja na mapandre na masista wa shirika la wa palotini kutoka jimbo katoliki la Singida.
Mashemasi hao wa shirika la wapalotini ni George Kimina,Faustini Fransis,Gonzaga Mtaawe,na Mikaeli Muhia.
Ushemasi ni mashuhuda wa utakatifu wa watu wa Mungu unaopata chimbuko lake katika maisha ya Sala za Kanisa, Tafakari ya Neno la Mungu na Nidhamu katika maisha ya Utii, Useja na Ufukara kama kielelezo makini cha ufuasi wa Kristo kwa njia ya maisha ya wakfu.
Monday, October 28, 2019
Askofu Msaidizi awasimika Mashemasi wapya,awataka wakamtumikie Mungu
Tags
# Top News
About Sultan Mapigo
SULTAN MAPIGO: Kuwa wa kwanza kuhabarika, Tafadhari usisahau kusubscribe kushare na kucomment
Top News
Tags:
Top News
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment