Adbox

Thursday, September 5, 2019

Nigeria kuwarudisha kwa ndege bure raia wake waishio Afrika Kusini

Wizara ya Mambo ya nje nchi Nigeria imetangaza kuwa shirika ya ndege ya la ‘Air Peace’ limejitolea kutuma ndege zake kwenda Afrika Kusini kesho Ijumaa ili kuwahamisha raia wa Wanigeria wanaotaka kurudi nchini, bila malipo yoyote.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Nigeria, Geoffrey Onyeama amewaambia wanahabari siku ya jana kuwa kulingana na taarifa zilizowafikia, hakuna raia wa Nigeria aliyepoteza uhai kwenye ghasia zinazoendelea.

"Kwa ujumla unashauriwa kuwajulisha jamaa zao waishio huko Afrika Kusini kutumia fursa hii ya kupendeza." aliesema.

Nchi ya Afrika Kusini katika miji mikubwa imekumbwa na vurugu kufuatia raia wa kigeni wanaofanya biashara kufanyiwa fujo na vijana ambao wanadai nafasi zao za ajira zimechukuliwa na wageni.

No comments:

Post a Comment

Adbox