Adbox

Friday, August 9, 2019

Hitimisho Nane Nane Nyakabindi Simiyu Kitaifa, NBC yaitaja TCCIA

Hivi ndivyo Sherehe za 88 Nyakabindi Simiyu zilivyohitimishwa jana Ambao waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano Mh Kassim Majaliwa alikuwa Mgeni Rasmi na Kuyasifu maonyesho haya kama ya ni Mfano na kutakaViwanja vya Nyakabindi Kubaki kama Shamba darasa na amesisistiza pasifungwe, Na ofisi za Idara ya Kilimo Halmashauri ya Bariadi kuahamia hapa pamoja na JKT na Jeshi la Magereza.


Kwa upande Mwingine Mdhamini Mkuu wa Maonyesho hayo Benki ya NBC imeitaja TCCIA kama Mshirika wao Muhimu katika kuwasaidia Wajasiria mali na wanaoanzisha Viwanda na Kilimo na wao kama Benki wamekuwa wakiwapa Ushirikiano,

Pia Maonyesho hayo ambayo yalihudhuriwa na Dk Meshack Kulwa Mjumbe wa Bodi na Mwenyekiti TCCIA Shinyanga ambaye alimwakilisha Kaimu Rais wa TCCIA Ndg Octavian Mshiu ambaye yeye alishiriki Kufungwa kwa Maonyesho ya Kimataifa ya SADC.

Dk Meshack akicheza ngoma maarufu ya Kisuma na baadhi ya Viongozi waandamizi wa Serikali pamoja na Wabunge.

No comments:

Post a Comment

Adbox