Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amepokea msaada wa vifaa mbalimbali kutoka benki ya NMB vyenye thamani ya sh. milioni 25.
Vifaa hivyo ni fremu 46 za madirisha ya alminium na vioo vyake, milango 18, mabati 56, misumari na mbao, kompyuta 10, madaftari 4,050 vyote vikiwa na thamani ya sh. milioni 25/-.
Akipokea msaada huo leo mchana (Jumapili, Julai 28, 2019) kwenye zahanati ya Nandagala, wilayani Ruangwa mkoani Lindi, Waziri Mkuu amewashukuru viongozi wa benki hiyo kwa kuamua kuchangia vifaa hivyo.
Akizungumza na wakazi wa kijiji cha Nandagala, Waziri Mkuu ambaye ni mbunge wa jimbo la Ruangwa, amesema mchango uliotolewa unamaanisha kazi ya kukamilisha jengo la wodi ya wagonjwa na vyumba vya madaktari ni lazima ifanyike haraka.
“Tunamshukuru Mkurugenzi Mkuu wa NMB kwa msaada huu mkubwa. Hii maana yake ni kwamba ni lazima tuharakishe kukamilisha jengohili ili tuanze kutoa huduma kwa wananchi wa Nandagala na wa vijiji vya jirani,” alisema.
“Tulianza na ujenzi wa zahanati kisha tukajenga jengo la upasuaji lenye wodi mbili. Moja ya wanaume na nyingine ya wanawake ambazo kila moja ina uwezo wa kulaza wagonjwa 20 kwa wakati mmoja.”
Jengo hili jipya ambalo tumelianza ujenzi wake, likikamilika litakuwa na uwezo wa kulaza wagonjwa 60. Pia kuna jengo lenye vyumba vya madaktari, vyumba vya upasuaji na vyumba vya kujifungulia.
Waziri Mkuu aliwataka wakazi hao wafikirie uwezekano wa kujenga wodi nyingine na pamoja na jiko ili wagonjwa watakaokuwa wanalazwa hapo, wapate mahali pa kupikiwa chakula.
Mapema, akitoa taarifa ya msaada huo, Mkuu wa Idara ya Huduma za Serikali katika benki ya NMB, Bi. Vicky Bishubo alisema kipaumbele cha benki hiyo kila mara ni kutatua changamoto za afya na elimu kwani sekta hizo ni nguzo kuu ya maendeleo kwa Taifa lolote.
“Vitu hivi (mabati, madirisha ya aluminium, kompyuta na madaftari) tunavyokabidhi leo ni moja ya ushiriki wetu katika maendeleo ya jamii na sisi kama benki inayoongoza Tanzania tunahakikisha jamii inayotuzunguka inafaidika kutokana na faida tunayoipata,” alisema.
Alisema kwa mwaka huu, NMB imetenga zaidi ya shilingi bilioni moja kwa ajili ya kuchangia maendeleo ya jamii ikiwemo kusaidia sekta ya afya na elimu. “Mpaka ninavyoongea leo, tayari tumetoa misaada yenye thamani ya zaidi ya millioni 600 kwa mwaka huu wa 2019 tu,” alisema.
Sunday, July 28, 2019
Waziri Mkuu apokea msaada wenye thamani ya Tsh. Mlioni 25.
Tags
# Top News
About Sultan Mapigo
SULTAN MAPIGO: Kuwa wa kwanza kuhabarika, Tafadhari usisahau kusubscribe kushare na kucomment
Top News
Tags:
Top News
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


No comments:
Post a Comment