Adbox

Friday, July 19, 2019

Rais Trump asema kuwa hakuna haja ya kuiadhibu Uturuki

Rais wa Marekani asema kuwa hakuna haja ya kuiadhibu Uturuki kutokana na  kununua kwake mfumo wa kujihami na makombora wa S-400 kutoka Urusi.

Rais wa Marekani akizungumza kuhusu Uturuki kununua mfumo wa kujihami na makombora wa S-400 kutoka nchini Urusi amejibu swali kuhusu mfumo huo kwa kusema kwamba Marekani haina haja kuiadhibu Uturuki kwa kununua mfumo huo.

Akiwa ikulu White House, Donald  Trump amehoji kana kwamba mataifa wanachama wa  jeshi la kujihami la Magharibi NATO yameanza kuwekeana vikwazo baina yao akimaanisha kuwa Uturuki ni mwanachama wa NATO ambalo linaashiria kuwa hakuna vikwazo vya aina yeyote dhidi ya Uturuki kwa kununua mfumo huo wa kujihami  na makombora kutoka nchini Urusi.

Rais wa Uturuki aliwahi kuzungumza kuhusu suala hilo  kabla ya kuondoka kujielekeza nchini Japan mwezi ulipita kushiriki katika mkutano wa G-20.

No comments:

Post a Comment

Adbox