"Ni mara kadhaa wamesema kuwa watatuma pesa kwa aji ya kukidhi mahitaji ya wakimbizi, ni nani ambae mnajaribu kumdanganya? hatuna haja ya pesa hiyo" amesema rais Erdoğan.
Mkutano huo na waandishi wa habari umefanyika Jumatatu.
Rais Erdoğan amesema kuwa Uturuki haina haja ya dola bilioni 1,1 ambazo Umoja wa Ulaya umefahamisha kuwa zitatumiwa kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya wahamiaji na wakimbizi kutoka Syria na mataifa mengine zaidi ya milioni nne waliopo Uturuki.
Rais Erdoğan amezungumza na waziri mkuu wa Bulgaria Boyko Borisov katika ziara yake nchini Uturuki.


No comments:
Post a Comment