Adbox

Thursday, March 12, 2020

Umoja wa Ulaya kutafakari marufuku ya usafiri ya Rais Trump

Umoja wa Ulaya umesema utautafakari uamuzi wa rais wa Marekani Donald Trump wa kupiga marufuku safari kati ya Marekani na nchi za umoja huo, kama sehemu ya mkakati wa serikali yake kupambana na virusi vya corona.

Marufuku hiyo ambayo haiihusishi Uingereza isio tena mwanachama wa Umoja wa Ulaya, itadumu kwa siku thelathini na itaanza kuheshimiwa kuanzia usiku wa kesho Ijumaa.

Kupitia mtandao wa Twitter, rais wa Baraza la Ulaya, Charles Michel amesema chochote kinachoweza kuvuruga uchumi kinapaswa kuepukwa.

Michel amesema Umoja wa Ulaya unafanya kila juhudi kuzuia kuenea kwa homa ya virusi vya corona, ijulikanayo kama COVID-19, na unasaidia katika utafiti juu ya kirusi hicho.

Marufuku ya usafiri iliyotangazwa na Rais Trump itawahusu watu wote wasio raia wala wakazi wa nchini Marekani, lakini Ikulu ya Marekani, White House imesema haijumuishi bidhaa.

No comments:

Post a Comment

Adbox