“Tanzania hatujapata corona ila hatuwezi kujiweka pembeni lazima tuchukue tahadhari, Corona inaua kwa haraka sana, Watanzania tusipuuze, tuchukue hatua za kujikinga, wanaopenda kusafirisafiri kama safari sio ya lazima usisaifiri na hatutotoa vibali vya Watu kusafiri hovyo” - JPM
“Narudia Watanzania tuchukue tahadhari, Waziri amesema tusishikane mikono, tusibusiane sasa sifahamu usiku watafanyaje ila napo unaweza kukwepa usibusu na mambo yakawezekana tu na ni raha tu, ila kiukweli corona ni hatari, haijafika Tanzania ila tujikinge”-JPM


No comments:
Post a Comment