Adbox

Thursday, March 12, 2020

Aliyekuwa na kesi ya uhujumu uchumi na kuachiwa kuachiwa kwa majadiriano na DPP akamatwa kwa utapeli

Mmoja wa washtakiwa wa kesi za uhujumu uchumi aliyeachiwa kwa utaratibu wa majadiliano kati yake na ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka nchini (DPP), amekamatwa akidaiwa kufanya utapeli.

Mtuhumiwa huyo anadaiwa kuchukua fedha kwa watu na kuwaambia kuwa anawapelekea maofisa wa ofisi ya DPP rushwa ili wawasaidie ndugu zao watoke mapema kwa utaratibu wa majadiliano.

Mkurugenzi wa Mashtaka nchini,  Biswalo Mganga amemtaja mtuhumiwa huyo ( jina limehifadhiwa) leo Alhamisi Machi 12, 2020 katika mkutano wake na waandishi wa habari, kwamba mtu huyo amekuwa akifanya vitendo hivyo katika maeneo mbalimbali.

"Anapofanya hivi inaonekana watumishi wa DPP na maofisa wa Serikali wanajiingiza katika rushwa. Alipofika tulimgundua na kutoa taarifa polisi na kumkamata, alikuwa amechukua Sh1.2 milioni kwa Edward Mtalima na baadhi ya watu wengine."


"Amechukua fedha hizi kwa madai anataka kumsaidia Mtalima ambaye ni mshtakiwa katika kesi namba saba ya uhujumu uchumi ya mwaka 2019. Hatuwezi kuvumilia upumbavu wa namna hii na atafikishwa mahakamani leo  akikabiliwa na mashtaka matatu," amesema Mganga.

Mganga amesema tayari ameshawapa maelekezo mawakili na hati ya mashtaka dhidi yake imeshaandaliwa na atasomewa leo huku akitoa onyo kwa wananchi wengine kutoingia katika vitendo hivyo na watakaobainika hatosita kuwachukulia hatua.

No comments:

Post a Comment

Adbox