“Maafisa uvuvi ninawaagiza hakikisheni mnasimamia sheria, na pia mtende haki, msimuonee mtu yeyote na watakaobainika na kujihusisha na vitendo vya rushwa tutawachukulia hatua za kisheria.” amesema Mhe. Ulega wakati akizungumza na wadau wa sekta ya uvuvi katika Kijiji cha Kigombe kilichopo Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga.
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Pangani Mhe. Jumaa Aweso ambaye ameshiriki katika kikao hicho amemuomba Mhe. Ulega kutatua changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo wavuvi zikiwemo za kupatiwa elimu juu ya sekta hiyo.
Akiwa katika kijiji cha Pangani Mashariki katika Wilaya ya Pangani alipotembelea Shamba la Serikali la Mivumoni Naibu Waziri Ulega amewataka wafugaji kutovamia mashamba ya serikali kwani kwa kufanya hivyo ni uvunjifu wa sheria na badala yake wafuate taratibu wanapohitaji maeneo kwa ajili ya malisho ya mifugo yao.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika siku ya kwanza ya ziara yake kwenye mikutano wilaya za Muheza na Pangani Mkoani Tanga, baadhi ya wadau wa sekta ya uvuvi wamemuomba Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega kuwatatulia changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo zikiwemo za wingi wa tozo, mikopo na elimu ya vifaa sahihi vinavyotakiwa katika shughuli za uvuvi ili kujiepusha na vitendo vya uvuvi haramu bila kukusudia.


No comments:
Post a Comment