“Utaratibu huu utaondoa mlundikano wa Kwacha upande wa Tanzania. Kama mnavyojua, Wananchi wa Zambia wananunua bidhaa na huduma kwa wingi kutoka Tunduma kwa kutumia Kwacha wakati Watanzania hawawezi kununua vitu kutoka upande wa Zambia (Nakonde) kwa kutumia Shilingi. Kwa sababu hiyo kunakuwa na Kwacha nyingi upande wa Tanzania ambazo hatimaye zinaishia mikononi mwa wauzaji wasio rasmi”
Urasimishaji huo unategemewa kuchochea shughuli za kiuchumi kwa kuwaondolea wananchi gharama za kubadili fedha kwani kuanzia sasa watauza na kununua kwa kutumia Kwacha na Shilingi kwa pamoja.
“Ushiriki wa Benki zetu hapa Mpakani katika kununua na kuuza Kwacha na Shilingi kunawapatia wananchi huduma salama za ubadilishaji wa fedha, ambapo wataepusha hatari ya Wananchi kupewa fedha bandia. Pia benki zitatoa viwango sahihi vya ubadilishanaji wa Kwacha na Shilingi hivyo kulinda thamani ya fedha zetu”, aliongeza.
Mhe. Irando alisema kuwa tukio hilo litaimarisha ushirikiano wa kihistoria kati ya Serikali ya Zambia na Tanzania na kuboresha hali ya maisha ya wananchi kwa kurahisisha shughuli mbalimbali za kiuchumi.
Uzinduzi wa utaratibu huo ni utekelezaji wa Hati ya Makubaliano (MOU) iliyosainiwa tarehe 21 Septemba 2018, kama jitihada za serikali ya Zambia na Tanzania za kumaliza changamoto ya muda mrefu ya biashara holela ya fedha za kigeni katika mpaka wa Tunduma na Nakonde.





No comments:
Post a Comment