Adbox

Wednesday, February 5, 2020

CCM Lindi yaingilia kati mgogoro wa ardhi, yatoa agizo kwa manispaa

Na Ahmad  Mmow, Lindi.

Chama Cha Mapinduzi  (CCM), mkoani Lindi   kimetoa siku saba kwa viongozi wa  watendaji wa Manispaa  ya  kumaliza mgogoro wa ardhi kati ya  mwananchi wa kijiji cha  Mningula  na mwekezaji

Agizo hilo limetolewa na katibu wa chama cha mapinduzi mkoa wa Lindi  Innocent Nanzaba baada ya wakulima 139 kufika kufika ofisi za chama kuomba msaada  kwa chama hicho kiingilie kati mgogoro huo ambao unaweza kuvuruga amani kwa wakazi wa kijiji hicho

Nanzaba Alisema amepokea ujumbe wa wakulima 139 ambapo umewakilishwa na wakulima 13 kutoka kijiji cha Mnengula kata ya Mnolela wamelalamikia  watendaji na uongozi wa Manispaa ya Lindi kugawa eneo lao kwa mwekezaji na kukwamisha shughuli za wakulima  hao kuendekea na kilimo.

Alisema CCM inatambua kuwepo kwa migogoro mingi ya ardhi inayosababishwa na baadhi ya watendaji wasio waadilifu na waaminifu ambao wanatumia ofisi zao kuni

jinufahmisha bila kukumbuka  kuwa  wao ni wasaidizi  wa Rais wa kutatua kero za wananchi

"Tumepokea malalamiko ya wakulima kuhusu mgogoro wao na mwekezaji  CCM itatembea eneo hilo na kulifanyia kazi  ili kutatua huo mgogoro  maana sisi tumekuja kumsaidia Rais wetu ambae ndie Mwenyekiti wa Chama  kazi,na hatupendi kuona wananchi wanapeleka lalamiko yao wakati  wa ziara za viongizi wa  juu akiwemo  rais kwa mabango  nawaomba watendaji kuumaliza mgogo huo kwa muda wa siku saba baada ya hapo chama kitachukua uamuzi"alisema  Nanzaba

Alisema cha mapinduzi hakitakubali kuona wananchi wanyonge  wakinyanyaswa na kubuguziwa  na watu wachache kwa maslahi binafsi kwa madai ya kuwa wao ni wawekezaji ,CCM inatambua umuhimu wa wawekezaji lakini kwa wale wanaotambua  utu wa wao na kufuata utaratibu uliwekwa.

Salumu  Nanokori Alisema watendaji wa  serikali ya wilaya  imeonekana  wanamaslai na mwekezaji kwani wameamua kufumbia macho suala la  mgogoro huo hali iliyosasabisha wananchi kukiomba chama cha mapinduzi  kuingilia kati kwa lengo la kutatua mgogoro huo ili wananchi waendelee na uzalishaji  kwa kuendelea kuendesha kazi yao ya  kilimo ili kuwafanya  waweza kuepuka na balaa la njaa.

Ili tatizo linashindwa kutatuliwa inaonyesha kuna baadhi ya  watendaji wananufaika  ndiyo maana wananchi tunatishwa na  tutakamatwa na polisi tunawekwa ndani bila sababu aluekeza  Salumu.

Alisema kuwa eneo hilo la zaidi ya hekari 350  Manispaa ya Lindi imempa mwekezaji wakati wakulima wa kijiji cha Mningula  jimbo la Mtama walikuwa wanaendesha shughuli za kilimo kwa muda mrefu

Katibu mwenezi CCM kata ya Mnolela Juma Bakari alisema  kuwa wananchi wa eneo hilo wameteseka kwa muda mrefu  ikiwemo kukamatwa na polisi na  kuwekwa rumande bila ya ufumbuzi wa suala hilo , mpaka wanalifikisha Ccm ngazi zingine wameshiindwa  kulitafutia ufunbuzi wa kudumu

 Bakari alisema  kuwa baada ya kukosa suluhisho la mgogoro kwenye ngazi ya watendaji akiwa na pamoja na ofisi ya mkuu wa wilaya ya Lindi   wakulima hao wameamua  walikwenda ofisini kwake nakuomba msaada  wa kutafuta ufumbuzi wa mgogoro wao wa muda mrefu ulisababisha baadhi ya wananchi  kusimamisha shughuli  zao za kilimo ndipo alipowafikisha ccm mkoa kutoa malalamiko yao.

Zainabu Saidi   ambae ni miongoni mwa  wananchi waliko kwenye  mgogoro huo alisema    wamemuomba  katibu  huyo wa CCM mkoa  kutatua mgogoro huo ambao umeonekana kudumu kwa muda wa zaidi ya miaka mitatu wakishindwa kufanya shughuli za kilimo.

Zainabu alisema  mgogoro umesababisha wananchi kushindwa kufanya kazi za kilimo kwenye eneo hilo pia umekuwa ukiwanyima amani kwani mara nyingi wamekuwa wakikamatwa na jeshi la polisi na kuwekwa ndani kwa madai wanaendesha shughuli za kilimo kwenye eneo la mwekezaji.

No comments:

Post a Comment

Adbox