Adbox

Thursday, February 27, 2020

CAF: Viwanja vya mpira Zimbabawe havitimizi viwango kuchezwa mechi za kimataifa

Shirikisho la soka barani Afrika CAF limetangaza jana kwamba viwanja vya Zimbabwe havitimizi viwango vinavyoruhusu kuchezwa mechi za kimataifa.

Tangazo hilo ni pigo kubwa dhidi ya juhudi za Zimbabawe za kutaka kutambuliwa kimataifa. Jumuiya ya mpira wa miguu ya Zimbabwe ZIFA imesema walipokea barua hiyo na walifadhaika.

Zimbabwe italazimika kutafuta kiwanja mbadala cha kucheza mechi ijayo dhidi ya Algeria.

 Msemaji wa jumuiya hiyo, ZIFA Xolisani Gwesela amesema watalazimika kama taifa kushirikiana ili kutimiza viwango vinavyohitajika.

No comments:

Post a Comment

Adbox