Pamoja na mambo mengine, mazungumzo hayo yalijadili mambo mbalimbali ikiwemo kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia baina ya Tanzania na Kuwait kupitia Nyanja mbalimbali ikiwemo uwekezaji wa miradi na biashara pamoja na uundwaji wa tume ya kudumu ya pamoja ya ushirikiano.
Aidha, Mhe. Balozi Alsehaijan alitumia fursa hiyo kumkabidhi Katibu Mkuu, Balozi Ibuge salamu za rambirambi kufuatia ajali zilizotokea hapa nchini hivi
karibuni.
Kwa upande wake Balozi Ibuge, alimweleza Mhe. Balozi Alsehaijan umuhimu wa kuendeleza jiji la Dodoma na kumkaribisha jijini Dodoma.
Mazungumzo hayo yamefanyika siku moja baada ya Ubalozi wa Kuwait nchini Tanzania kusheherekea miaka 59 ya Uhuru wake na miaka 29 ya ukombozi wa taifa hilo yaliyofanyika jana jijini Dar es Salaam.


No comments:
Post a Comment