Na Thabit Madai,Zanzibar.
Waziri wa Katiba na Sheria Zanzibar, Khamis Juma Maalim ameitaka kampuni ya Advent Construction Limited kutoka jijini Dar es Salaam kukamilisha kwa muda waliokubaliana Ujenzi wa Jengo la Mahakama kuu iliyopo Tunguu Mkoa wa Kusini.
Amesema Ujenzi huo utachuuwa kipindi cha mwaka Mmoja ambapo Jengo hilo linatarajiwa kumalizikwa ifikapo mwaka 2020.
Hayo aliyaeleza huko Mahakama Kuu Vuga wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya ghafla ya kutiliana saini na Kampuni ya Advent Construction ambayo inayotarajia kujenga Mahakama mpya Tunguu Mkoa wa Kusini Unguja.
Alisema kitendo cha kusaini mkataba huo ni muhimu sana ikiwa ni Utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ikiwemo kusimamia na kuimarisha haki ili wananchi wapate haki za kusimamia kesi zao.
Aliwataka kujenga jengo lenye ubora na kukamilisha kwa muda uliopangwa ili wawe na jengo la kisasa na waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi na kupata Mahakama iliyo nzuri Zanzibar ambapo inatarajiwa kumalizika hapo mwakani kabla ya Dkt Shein kumaliza uongozi wake ikiwa ni miongoni mwa ahadi zake.
Pia alisema sheria ya msaada ishatungwa kwa lengo la kuandaa mazingira yaliyo mazuri kwa wananchi kupata haki zao kwa urahisi.
Hivyo aliwaomba wakandarasi hao kujenga jengo lenye ubora na kiwango madhubuti ili liweze kudumu kwa muda mrefu na kutarajia likimaliza litasaidia Serikali katika utendaji wake.
“Tunaomba jengo hili lijengwe kwa kiwango kilicho bora ili kuweza kudumu kwa muda mrefu na kuepuka kujenga jengo bila ya kiwango” alisema Waziri huyo.
Nae Jaji Mkuu Omar Othman Makungu aliwataka wakandarasi hao kuhakikisha wanajenga Mahkama iliyo ya kupendeza ili na sie tuwe na Mahakama iliyo nzuri yenye sifa kwa Zanzibar na kufanya wafanyakazi kila kitendo kinapata sehemu ya kufanyia kazi kwa nafasi.
Alisema wanaishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kujiandaa kutujengea jengo la Mahakama mpya kwa lengo la kutuimarishia miundo mizuri ya utendaji wa kazi kwa kila sekta.
“Tunashukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuweza kutaka kutujengea jengo hili kwani jengo hili sasa lishakuwa dogo halikidhi haja kwa wafanyakazi hivyo likimalizika huko tutaweza kufanya kazi zetu katika mazingira mazuri”, alisema Jaji huyo.
Monday, October 21, 2019
Home
/
Top News
/
Waziri aitaka kampuni ya Advent Constructio limited kukamilisha ujenzi wa Mahakama kuu
Waziri aitaka kampuni ya Advent Constructio limited kukamilisha ujenzi wa Mahakama kuu
Tags
# Top News
About Sultan Mapigo
SULTAN MAPIGO: Kuwa wa kwanza kuhabarika, Tafadhari usisahau kusubscribe kushare na kucomment
Top News
Tags:
Top News
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment