Na Thabit Madai,Zanzibar.
Waziri wa Afya Zanzibar Hamad Rashid Mohamed ameitaka Jumuiya ya Madaktari Wanafunzi Tanzania {TAMSA) kufanya kazi kwa kufuata maadili ili kuepuka kwenda kinyume na utaratibu wa udaktari.
Hayo aliyasema huko katika Uwanja wa Mapinduzi Square wakati alipofunga zoezi la huduma ya afya kwa wananchi wa Zanzibar lililoandaliwa na Jumuiya ya Madaktari Wanafunzi Tanzania.
Alisema suala la maadili ya kazi hasa kwa wale madaktari wanafunzi hupaswa kuzingatia kutokana na kanuni za kazi kwani kuepuka maadili kunateremsha hadhi ya udaktari.
“Kuitumia lugha nzuri kwa mgonjwa kunampa matumaini ya kupata tiba nzuri katika maradhi aliyonayo pindipo akitolewa maneno makali huchangia kumuadhiri kisaikolojia na kumkatisha tamaa”alisema Waziri.
Alisema sambamba na maadili katika kazi pia amewataka madaktari na wauguzi kuwa wazalendo katika ufanyaji wa kazi zao si tabia njema kuisambaza katika mitandao ya kijamii.
Alisema kwa upande wa Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya mnazi mmoja Madaktari wameweza kujirekebisha na kutoa huduma iliyo bora kwa wagonjwa licha ya kuwa kunajitokeza baadhi ya vituo vya afya bado wanaitumia lugha chafu kwa wagonjwa .
Aidha alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu imefanya juhudi ya kujenga vituo vya afya katika sehemu tofauti ili mwananchi waweze kupata huduma hiyo kwa ukaribu.
Hata hivyo aliitaka jumuiya Madaktari Wanafunzi Tanzania kuengeza juhudi ya wataalamu kutokana na mahitaji yaliopo hivi sasa ya teknolojia mpya za vifaa tiba zinahitaji watendaji wengi na wenye sifa za kuweza kuzitumia.
Alisema licha ya ununuzi mkubwa wa mashine mpya za vifaa tiba pia kunaupungufu wa wataalamu katika hospitali za Zanzibar.
Nae Makamo ya Rais wa Jumuiya ya Madaktari Wanafunzi Tanzania alisema lengo ni kuwasogezea wananchi huduma za afya iliyobora na kuwafanyia uchunguzi wa maradhi mbalimbali ili waweze kupatiwa tiba kwa haraka pindipo wakigundulika mapema.
Alisema kuwapatia matibabu wananchi kutasaidia kupunguza kiwango cha maradhi kwa kupatiwa ushauri wa kidaktari mapema na kutasaidia watanzania kufikia katika afya bora nchini
Aliweza kuzishukuru taasisi 17 zilizowaunga mkono kufanikisha zoezi la upimaji afya ikiwemo wizara ya afya,
Zoezi hili la upimaji wa afya ni la siku tatu ni la mara ya pili kufanyika Zanzibar awali lilifanyika mnamo mwaka 2014.
Monday, October 21, 2019
TAMSA yatakiwa kufanya kazi kwa kufuata maadili
Tags
# Top News
About Sultan Mapigo
SULTAN MAPIGO: Kuwa wa kwanza kuhabarika, Tafadhari usisahau kusubscribe kushare na kucomment
Top News
Tags:
Top News
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment