Timu Teule za Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) zimewasili salama Wuhan nchini China amabapo zinatarajia kushiriki mashindano ya dunia ya majeshi kuanzia tarehe 18 mwezi huu.
Mara baada ya kuwasili, bendera ya Tanzania ilipandishwa kuashiria kuwepo kwa timu za Tanzania kati nchi 110 zinazoshiriki mashindano hayo mwaka huu.
Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa bendera mkurugenzi wa michezo jeshini Kanali Erasmus Bwegoge alisema ni faraja kupandisha bendera ugenini sasa ni wakati muafaka kuitangaza vyema kwa kuibuka na ushindi.
Kwa upande wake mkuu wa msafara Brigedia Jenerali Selemani Mzee amesema kikosi kiko imara na wachezaji wote wako timamu na hakuna majeruhi na wanachoendelea nacho ni mazoezi na kusubiria kupangwa kwa mechi.
Wachezaji wa Tanzania wamekuwa kivutio kila kona huku kaulimbiu ya ‘HAPA KAZI TU’ imekuwa ikitamaniwa kutamkwa na watu mbalimbali wakiwemo wachina huku Rais John Magufuli akiwa kivutio kwa kazi zake nzuri ambazo amekuwa akizifanya kwa maendeleo ya nchi.
Friday, October 18, 2019
Timu ya JWTZ yawasili China, Bendera ya Taifa yapandishwa
Tags
# Top News
About Sultan Mapigo
SULTAN MAPIGO: Kuwa wa kwanza kuhabarika, Tafadhari usisahau kusubscribe kushare na kucomment
Top News
Tags:
Top News
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


No comments:
Post a Comment