Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu amewataka Watumishi wa Hifadhi ya Taifa Arusha kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia Sheria bila kuwanyanyasa wananchi.
Aidha, Kanyasu amewataka wananchi kuzingatia sheria za uhifadhi ikiwa pamoja na kushiriki katika kulinda Hifadhi hiyo
Ametoa kauli hiyo leo wakati alipokuwa akizungumza na Wananchi wa Kitongoji cha Momela kata ya Ngarenanyuki katika wilaya ya Arumeru mkoani Arusha.
Hatua hiyo inakuja kufuatia mgogoro wa ardhi uliodumu kwa muda wa miaka 30 baina ya wananchi hao na Hifadhi ya Taifa ya Arusha.
Wananchi wa Kitongoji cha Momella wanadai kuwa mwaka 1992,Hifadhi ya Taifa ya Arusha ilimega hekta 600 ya ardhi ambayo ilikuwa inamilikiwa na Kitongoji hicho, Licha ya wananchi hao kushinda kesi mahakamani hawajarudishiwa Ardhi yao hadi leo.
Kanyasu amewaeleza wananchi hao kuwa Serikali inautambua mgogoro huo na ni miongoni mwa migogoro 1000 inayofanyiwa kazi na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Kufuatia hali hiyo, Mhe.Kanyasu amewataka wananchi hao kuendelea kuwa watulivu hadi pale Serikali itakapotoa orodha ya majina ya vijiji na vitongoji ambavyo vitakuwa vimeondolewa kwenye Hifadhi nchini.
Katika hatua nyingine, Mhe.Kanyasu amewaatahadharisha wakazi wa Kitongoji hicho kutokuingiza mifugo ndani ya Hifadhini kwa kisingizio cha mgogoro huo.
Kwa Upande wake Mbunge wa Arumeru, Dkt.John Pallangyo amewasihi wananchi kuendelea kuzingatia sheria za Uhifadhi huku wakisubili orodha ya majina ya vijiji na vitongoji vitakavyotangazwa kuondolewa katika Hifadhi nchini.
”Natambua mna uchungu na mmeteseka kwa muda mrefu juu ya Mgogoro huu, Niwahakikishie Waziri kawasikia na kajionea mwenyewe” alisisitiza Mhe.Pallangyo.
Awali akizungumza kwenye mkutano wa hadhara, Mwenyekiti wa Kitongoji hicho, Anael Nko amemueleza Naibu Waziri huyo kuwa kwa muda miaka 30 sasa maisha yao yameendelea kuwa ya uhasama kati yao na Hifadhi.
Kufuatia hali hiyo, Mwenyekiti huyo amemuomba Naibu Waziri kuumaliza mgogoro huo kwani umekuwa ukiwarudisha nyuma kimaendeleo.
Mbali na hilo, Mwenyekiti alisema licha ya mgogoro huo wanaihitaji Hifadhi kwa vile licha ya changamoto hizo wanazokumbana nazo Hifadhi hiyo imekuwa na manufaa makubwa sana kwao.
Monday, October 28, 2019
Serikali yasisitiza mahusiano mema kati ya wananchi na hifadhi
Tags
# Top News
About Sultan Mapigo
SULTAN MAPIGO: Kuwa wa kwanza kuhabarika, Tafadhari usisahau kusubscribe kushare na kucomment
Top News
Tags:
Top News
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment