Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amewataka Wakuu wa mikoa nchini kuhakikisha wanaharakisha uanzishwaji Ofisi za Ardhi za mikoa ili kusaidia upatikanaji huduma za ardhi katika mikoa hiyo.
Lukuvi alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki mkoani Tanga wakati alipokagua ofisi zinazotarajiwa kuwa za ardhi katika mkoa huo ikiwa ni utekelezaji wa agizo alilolitoa la kuanzisha ofisi za ardhi kila mkoa kwa ajili ya kusogeza huduma za ardhi kwa wananchi.
Katika Mkutano wa Wataalamu wa sekta ya ardhi uliofanyika hivi karibuni jijini Dodoma Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi alitangaza kuanzisha ofisi za ardhi katika kila mkoa ili kurahisisha huduma za sekta hiyo ambapo sasa zinapatikana katika Kanda tisa ikiwemo ile Maalum ya Morogoro.
Lukuvi alisema, uharakishwaji uanzishaji ofisi za ardhi katika mikoa utasaidia wananchi kupata huduma za ardhi katika mikoa yao tofauti za sasa ambapo hulazimu baadhi yao kutembea umbali mrefu kufuatilia nyaraka ofisi za kanda jambo aliloeleza linawakatisha tamaa.
Alimpongeza mkuu wa Tanga Martine Shighela kwa kuwa Mkuu wa mkoa wa kwanza kukubali na kupokea agizo la kuanzishwa ofisi hizo za ardhi mapema kwa lengo la kuhakikisha migogoro ya ardhi inaondolewa katika mkoa wake.
Tuesday, September 3, 2019
Waziri Lukuvi awapa kazi hii Wakuu wa Mikoa nchini
Tags
# Top News
About Sultan Mapigo
SULTAN MAPIGO: Kuwa wa kwanza kuhabarika, Tafadhari usisahau kusubscribe kushare na kucomment
Top News
Tags:
Top News
Subscribe to:
Post Comments (Atom)



No comments:
Post a Comment