Waziri wa Katiba na Sheria nchini Tanzania, Balozi Augustine Mahiga amesema Serikali inayojisifia kuzingatia utawala bora lazima itoe fursa ya wananchi kupata taarifa sahihi huku akisema kuwa taarifa hizo ni zile zinazomuwezesha raia kuchukua uamuzi bora na sahihi.
Ametoa kauli hiyo leo Mkoani Morogoro katika maadhimisho ya kimataifa ya siku ya upataji taarifa ambayo kitaifa yameandaliwa na mtandao wa vyombo vya habari vya jamii Tanzania (Tadio) kwa ufadhili wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (Unesco).
Balozi Mahiga amesema upatikanaji na utoaji wa taarifa ni sehemu ya utawala bora unaojumuisha masuala mbalimbali ikiwemo demokrasia, kutaka taarifa kutumika vyema kwa manufaa ya wananchi.
"Unaweza kuchukua uamuzi mbaya kama huna taarifa ya kutosha katika jambo fulani, hivyo tukisema kupata taarifa ni pamoja na kutoa mchango katika kutengeneza Serikali bora," amesema.
Amebainisha kuwa taarifa ni sawa na panga lenye makali pande zote mbili, upande mmoja linaleta haki na mwingine kuleta uvunjifu wa amani.
Saturday, September 28, 2019
Balozi Mahiga atoa neno kuhusu Utawala bora
Tags
# Top News
About Sultan Mapigo
SULTAN MAPIGO: Kuwa wa kwanza kuhabarika, Tafadhari usisahau kusubscribe kushare na kucomment
Top News
Tags:
Top News
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


No comments:
Post a Comment