REUTERS
Mwanaharakati msomi wa Uganda Dkt. Stella Nyanzi amehukumiwa kifungo cha miezi 18 jela.
Nyanzi alipatikana na hatia ya unyanyasaji wa kimtandao pamoja na mawasiliano ya udhalilishaji dhidi ya rais Yoweri Museveni na familia yake.
Dr. Nyanzi alikataa kumsikiliza hakimu akisoma hukumu dhidi yake na badala yake kufanya vurugu kwa kuvua nguo na kuonesha sehemu ya mwili wake.
Mwanaharakati huyo hakuwa mahakamani lakini hukumu dhidi yake ilitolewa kupitia video link kutoka jela.
Wakati kesi ikiendelea Bi. Stela alikataa kuomba dhamana na amekuwa katika gereza kuu la Uganda la Luzira kwa miezi minane.
Sasa atazuiliwa gerezani kwa miezi tisa zaidi.

Nchini Uganda Uganda, Bi Nyanzi amekua sura na sauti ya matumizi ya lugha chafu katika upinzani dhidi ya kile anachokiita serekali mbaya.
Haoni haya ya kuandika maneno ambayo wengi wanayaona kama ni ya aibu.
Nyanzi ni mtafiti wa masuala ya jamiina msomi na kabla ya kuanza kampeni yake ya matusi kupitia kwenye mitandao ya kijamii aliwa ni mwalimu katika chuo kikuu cha umma nchini Uganda cha Makerere.
Mashtaka hayo chini ya ya sheria ya matumizi mabaya ya kompyuta ni jaribio latika utekelezwaji wa sheria ya uhalifu wa mtandaoni inayokosolewa.
Wengi miongoni mwa washukiwa wa unyanyasaji wa mtandaoni , wamekuwa hata hivyo wakishutumiwa kwa kumshambulia rais Museveni.

No comments:
Post a Comment