Adbox

Saturday, August 17, 2019

Rais Magufuli atoa ahadi kwa wanachama wa SADC

Rais wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ameahidi kushirikiana na nchi zote, wanachama wa SADC.

Rais ametoa agizo hilo leo katika Ukumbi wa JNICC, jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 39 wa SADC ambapo amesema "Kama mjuavyo, mkutano huu unafanyika ikiwa imepita miaka 20 tangu Baba wa taifa letu Mwalimu Nyerere ambaye alikuwa miongoni mwa waanzilishi wa jumuiya hii afariki dunia."

"Hivyo basi tunaahidi kushirikiana na nchi zote, wananchama wa SADC kuhakikisha kwamba kupitia mkutano huu, ndoto na mawazo ya Baba yetu wa taifa, pamoja na viongozi wengine waanzilishi wa jumuiya hii yanaendelea kutekelezwa kwa vitendo,” Rais Magufuli.

No comments:

Post a Comment

Adbox