Adbox

Friday, August 30, 2019

Ahukumiwa miaka ishirini Jela

Na.Rahel Nyabali, Tabora.

Mahakama  ya  hakimu  mkazi  mkoa  wa  Tabora  imemuhukumu  Fabian  Francis  Mkazi  wa  Kaliua,  kutumikia  kifungo cha miaka ishirini na miezi sita jela baada ya kupatikana  na hatia  ya  kukutwa na nyara za Serikali ndani ya hifadhi ya msitu wa Ugalla wilayani Kaliua mkoani Tabora.

Awali katika mwenendo wa shauri hilo Wakili upande wa Jamhuri Tito Mwakalinga aliieleza  mahakama kuwa mshitakiwa Fabian Francis alikamatwa ndani ya hifadhi ya ugalla wilayani Kaliua  eneo la Upango mnamo tarehe 2 January 2019 akiwa na nyama ya wanyama wa Porini yenye  thamani ya zaidi ya shilingi milioni nne na silaha ndogo kinyume cha Sheria ya hifadhi ya  wanyamapori namba tano ya mwaka 2009.

Akisoma hukumu katika shauri hilo la uhujumu uchumi namba sita la mwaka 2019 Hakimu mkazi  mfawidhi mkoa wa Tabora Chiganga Mashauri Tengwa amedai kuwa maamuzi hayo ya mahakama  yamefikiwa baada ya kupitia maelezo ya pande zote mbili na kujiridhisha pasipo shaka yoyote kwamba mshitakiwa Fabian Francis amehusika kutenda makosa mawili baada ya kukutwa ndani ya  hifadhi ya msitu wa Ugalla akiwa na nyara za Serikali nyama ya wanyamapori.

No comments:

Post a Comment

Adbox