Askari Magereza katika Gereza la Butimba wamuomba Rais Magufuli vitendea kazi yakiwemo magari.
Askari hao wamesema hawana magari na wamekuwa wakihatarisha maisha yao kwa kuwabeba mahabusu na wafungwa katika magari mabovu sanjari na mkuu wa gereza kutokuwa na gari linaloweza kumsaidia katika kazi zake za utendaji.
" Mheshimiwa Rais ni aibu mno na sisi ni wanyonge katika masuala ya usafiri, tena Tanzania nzima, tunaomba utusaidie kutupatia magari ikibidi coastal na makazi yetu hayako katika hali nzuri." Mmoja wa askari Magereza
Baada ya maombi hayo, Rais Magufuli naye akajibu, "Kwa maaskari Magereza nimesikia kilio chenu ninyi hamna tofauti na majeshi mengine na hamuwezi mkawa mnafanya kazi kwa kulalamika, hakikisheni hawa wafungwa hawaingii na simu gerezani, nyembe, wanaofanya biashara na hawa wafungwa wasifanye.” .
Tuesday, July 16, 2019
Home
/
Habari
/
Mh. Rais ni aibu mno na sisi ni wanyonge katika masuala ya usafiri - Askari Magereza
Mh. Rais ni aibu mno na sisi ni wanyonge katika masuala ya usafiri - Askari Magereza
Tags
# Habari
About Sultan Mapigo
SULTAN MAPIGO: Kuwa wa kwanza kuhabarika, Tafadhari usisahau kusubscribe kushare na kucomment
Habari
Tags:
Habari
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


No comments:
Post a Comment