Adbox

Friday, July 19, 2019

Julius Mtatiro aapishwa kuwa DC wa Tunduru

Mkuu mpya wa Wilaya ya Tunduru, Julius Mtatiro ameapishwa leo Julai 19, 2019. Hafla ya kuapishwa kwa Mtatiro imeongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Christina Mndeme na kuhudhuriwa pia na wakuu wengine wa wilaya katika mkoa huo.

Julai July 2019 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli alimteua Julius Mtatiro kuwa mkuu wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma.

Mtatiro alichukua nafasi ya Juma Zuberi Homera ambaye ameteuliwa kuwa mkuu wa mkoa wa Katavi.

No comments:

Post a Comment

Adbox