Adbox

Thursday, March 19, 2020

Watu sita washitakiwa kwa mauaji ya mwandishi habari Brazil

Ofisi ya mwanasheria mkuu nchini Brazil imewafungulia mashtaka ya mauaji watu sita waliokuwa maafisa wa jeshi wakati wa utawala wa kidikteta. Watu hao wanatuhumiwa kumuua mwandishi habari maarufu, Vladimir Herzog Oktoba 25, mwaka 1975.

 Herzog alikufa wakati anashikiliwa kwenye kituo cha ujasusi cha jeshi baada ya kukamatwa na kuteswa.

 Wakati anauawa alikuwa na umri wa miaka 38. Akiwa mkurugenzi wa televisheni ya ''TV Cultura'', Herzog alikuwa akizungumza kwa uwazi na aliunga mkono demokrasia na alikuwa mwanachama wa chama cha Kikomunisti cha Brazil.

Uchunguzi wa kifo chake ulifunguliwa mwaka 1992, lakini ukafutwa na mahakama kwa kuzingatia sheria ya msamaha ya mwaka 1979. Uchunguzi wa kifo cha Herzog ulifunguliwa tena mwaka 2018.

No comments:

Post a Comment

Adbox