“Uchunguzi unafanyika kwa awamu, awamu ya kwanza ilimalizika na taarifa yake ilitolewa Januari 22, 2020 na sasa tunatoa awamu ya pili na ya tatu itatolewa baadaye.”
“Mpaka leo tumeokoa Sh8.8 bilioni ambapo awamu ya kwanza tuliokoa Sh4 bilioni na awamu ya pili tumeokoa Sh4.8 bilioni,” amesema.
Amesema miongoni mwa Sh8 bilioni zilizookolewa wahusika wamezirejesha wenyewe na baadhi yao wamezirejesha baada ya mahojiano na Takukuru.
Kuhusu hatua zitakazochukuliwa, Mbungo amesema kinachofanyika sasa ni busara kuwaongoza kukusanya fedha kwani wakimweka mtu ndani siyo kupata fedha lakini baadaye wahusika wanaweza kupelekwa mahakamni.


No comments:
Post a Comment