Nauli zilizopanda ni Dar es Salaam kwenda Dodoma kupitia njia ya Iringa.
Daraja hilo lililopo Gairo linalounganisha mikoa ya Dodoma na Morogoro lililosombwa na maji juzi saa 9:00 alasiri kufuatia mvu zinazoendelea.
Juzi kabla ya Serikali kufunga barabara hiyo mamia ya abiria na magari yalikwama eneo hilo huku baadhi wakilazimika kutumia njia mbadala.
Uchunguzi wa Mwananchi umebaini nauli kutoka Dar kwenda Dodoma kupitia Iringa ilikuwa Sh40,000 kutoka Sh22000 kwa basi daraja la kawaida; Sh28,000 hadi Sh45,000 daraja la kati; na Sh50,000 kutoka Sh35,000 daraja la maalumu (VIP) kupitia njia ya Iringa.
Umbali wa kutoka Dar-Iringa hadi Dodoma ni takriban kilomita 760, huku Dar-Moro hadi Dodoma ni kilomita 454.


No comments:
Post a Comment