Adbox

Friday, February 7, 2020

Waziri Haroun amewataka watoa huduma za kisheria kufanya kazi kwa uwadlifu

Na Thabit Madai, Zanzibar.

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Raisi, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Zanzibar, Haroun Ali Suleiman amewataka watoa huduma wa  msaada wa sheria Nchini kufanya kazi kwa uwadilifu na kuacha kufikiria  maslahi binafsi kutokana kuwa Wananchi  wanahitaji kutatuliwa changamoto zao kisheria.

Haroun amesema kuwa Wananchi wana Matumaini makubwa na watoa huduma wa msaada wa kisheria hivyo wanatakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia maadili na uwadilifu katika kazi zao.

Hayo ameyaeleza wakati akihutubia Wananchi katika Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Msaada wa Kisheria yaliyaofanyika leo katika Ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdul Wakili Kikwajuni Mjini Unguja.


Waziri Haroun alisema kwamba Jamii inakabiliwa na changamoto mbali mbali ambazo zinahitaji kutatuliwa kisheria hivyo wasaidizi wa Sheria wanatakiwa kutatua changamoto hizo  za jamii kwa kuzingatia uwadilifu nakuacha kufikiria maslahi yao binafsi.

Alisema wasaidizi hao wa Sheria   wanatakiwa kujikita zaidi katika kutoa msaada wa kisheria na si kufikiria kufanya biashara ya huduma wanazozitoa.

“Tambueni kuwa Jamii inamatumaini makubwa na nyinyi nendeni mukafanye kazi ya kuwasaidia katika changamoto ambazo zinawakabili, musifikirie kufanya biashara, toeni huduma hizo kwa uwadilifu kama inavyotakiwa” alisema Waziri Harouni.


Aliongeza kwa kufahamisha kuwa watoa huduma wa Msaada wa kisheria ni wajibu wao kutoa huduma hizo kwa kuzingatia  misingi ya  utawala bora.

“Kama munavyojua chini ya Uongozi wa Dk Shein utawala bora meimarika kwa kiasi kikubwa hivyo na nyinyi nendeni mukafanye kazi kwa kuzingatia maadili, uadilifu pamoja na Utawala bora” aliongeza kusema Waziri huyo.

Aidha  alifahamisha kwamba  Wananchi wanashindwa kupata haki zao kutokana na kuenea kwa  rushwa ambayo  inachangia  kwa kiasi kikubwa  kupotea  kwa haki za wananchi kwani watendaji wanaohusika huzifanya kazi zao kibiashara hali inayodumaza ustawi wa jamiii.

Katika Maelezo yake Waziri Haroun alieleza kuwa Mfumo wa usajli wa watoa huduma za msaada wa kisheria kwa njia ya kieletroniki  utaweza  kusaidia katika upatikanaji wa taarifa na takwimu kwa usahihi katika matukio ya udhalilishaji pamoja na madawa ya kulevya na migogoro ya ardhi ambayo yanawasumbua sana wananchi  ambao hawana uwelewa juu ya sheria.

Hata hivyo Waziri huyo alitoa wito kwa Mahakama,Jeshi la Polisi,Vituo vinavyotoa huduma za kisheria na Chuo cha Mafunzo  kuwa waadilifu katika kazi zao ili kuwapatia haki zao wananchi  bila ya muhali na ubaguzi.

Kwa upande wake Waziri wa Katiba na Sheria Khamis Juma Mwalim alisema  Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali katika kuhakikisha wananchi wanapatia msaada wa kisheria kwa changamoto ambazo zinawakabil.



Alisema moja ya jitihada hizo ni kuanzisha mfumo ambao utawawezesha watoa huduma za msaada wa kisheria Unguja na pemba kutambulikana na Sehumu walipo.



Waziri Mwalimu alifahamisha kuwa  kila mwananchi  anafursa  sawa kwenye haki  hivyo  mfumo huo ni nguzo imara katika ustawi wa kupata haki  zao katika  kuleta  maendeleo kwa wote bila ya ubaguzi.



Mapema Mkurugenzi Idara ya Msaada wa kisheria  Zanzibar Hanifa Ramadhan Said alisema  kesi za udhalilishaji,jinai,madawa ya kulevya  hazina msaada wa kisheria jambo linalopelekea  vitendo hivyo kuongezeka  hivyo uwepo wa mfumo wa msaada wa kisheria utaweza kuleta mabadiliko katika upatiknaji wa haki kwa wananchi.



Alisema  tokea kuanzishwa kwa idara hiyo tayari mafanikio yameanza kupatikana kutokana na kuwepo kwa mashirikiano mazuri kutoka kwa wadau pamoja na taasisi mbalimbali zinazofanya kazi za kisheria.



Hanifa alisema kazi inayofanywa na wasaidizi wa msaada wa kisheria wa kutoa huduma kwa jamii  zinafanywa bila ya malipo  hivyo wananchi  watoe mashirikiano ya karibu na wadau wa sheria katika kupata haki zao za msingi.



Kwa upande wa  Mratibu wa Mfuko unaotoa ruzuku kwa watoaji wa msaada wa sheria (LSF) Joseph Magazi aliyomba  Serikali kuongeza  nguvu za kutoa elimu zaidi kwa wananchi ambao hushindwa kufika kwenye vyombo vya sheria  pindi  wanapopta  matatizo ambayo yanahitaji msaada wa sheria hasa yale ya udhalilishaji kwa watoto.



Alisema  Mfuko huo  hutoa ruzuku ili wananchi waweze kupatiwa  msaada kwa lengo la kupata haki zao ambazo wameshindwa kuzipata kutokana na uwezo wao mdogo.



Maadhimisho ya Wiki ya Sheria ni ya kwanza kuandaliwa na Wizara ya Katiba na Sheria chini ya Idara ya Msaada wa Kisheria.

No comments:

Post a Comment

Adbox