Adbox

Thursday, February 20, 2020

Rais wa Uturuki: Harakati za kijeshi mjini Idlib zinasubiri muda tu

Rais wa Uturuki amesema kwamba "ni suala la muda tu " kabla ya nchi yake kuanza harakati za kijeshi kuzuwia mashambulio ya jeshi la Syria dhidi ya eneo linalodhibitiwa na upinzani katika jimbo la Idlib.

Recep Tayyip Erdogan ameonya kuwa anaazimia kufanya mabadiliko katika eneo la mpaka na kulifanya kuwa sehemu salama "kwa garama yoyote ile".

Serikali ya Syria na washirika wake Urusi wamekataa madai yake ya kurudisha nyuma majeshi yake hadi kwenye uzio wa eneo la usitishaji mapigano lililoafikiwa mwaka 2018.

Uturuki: Syria 'itajuta' kwa kushambulia vikosi vyetu
Je muungano mpya wa Urusi, Uturuki na Syria unaiweka wapi Marekani?
Mapigano yamesababisha raia wapatao 900,000 wakiwemo watoto nusu milioni kuyakimbia makazi yao tangu Disemba 1.

Mamia wameuawa katika kipindi hicho, wengi wakiwa ni wahanga wa mashambulio ya wanajeshi wa serikali ya Syria na washirika wao kwa mujibu wa Umoja wa Matifa.

Watoto pia wanakufa kutokana na baridi, akiwemo mtoto mdogo mwenye umri wa mwaka mmoja msichana na mtoto mchanga wa kiume aliyekuwa na miezi saba.

"Uhasama sasa umefikia maeneo yenye msongamano wa watu. Watu wanakimbilia maeneo ya barafu kutafuta usalama ambao umekuwa mgumu zaidi,'' kwa mujibu wa msemaji wa Umoja wa mataifa.

Katibu mkuu wa umoja wa Mataifa António Guterres ametoa wito wa mapigano kusitishwa mara moja.

Zaidi ya watu 700,000, mkiwemo watoto 400,000 wamekimbia nyumba zao tangu mwezi Disemba
Idlib ni ngome ya mwisho ya waasi na wapiganaji wa jihadi ambao wamekua wakijaribu kumuondua madarakani rais wa Syria Bashar al-Assad tanga mwaka 2011.

Katika miaka ya hivi karibuni idadi ya watu waliosambaratishwa imeongezeka mara dufu hadi kufikia watu wapatao milioni tatu miongoni mwao watoto milioni moja.

Uturuki, ambayo inaunga mkono upinzani dhidi ya Bwana Assad na inaogopa kupokea wakimbizi wengi kutoka Syria, imepeleka wanajeshi wake katika vituo vya uangalizi mjini Idlib chini ya mkataba na Urusi ambao uliweka eneo lisilokuwa na mapigano- mkataba wa Sochi wa mwaka 2018.

Hata hivyo, imeshindwa kulizuwia jeshi la Syria kuchukua tena maeneo makubwa ya jimbo hilo kwa msaada wa mashambulio ya ndege za Urusi na wanamgambo wanaoungwa mkono na Iran.

Mashambulizi ya hivi karibuni ya serikali na hakikisho la kuvuka kwa raia kwenye mpaka wa kuingia Uturuki vimeyachochea jeshi la Uturuki kuanza kujiimarisha katika maeneo yake ndani ya Idlib tangu Januari. Maelfu ya wanajeshi na maelfu ya vifaru vya kijeshi viliwasili tangu wakati huo.

Mapema mwezi huu, baada ya wanajeshi kadhaa wa Uturuki kuuawa katika mashambulio ya makombora ambayo maafisa wa Uturuki walisema yalirushwa na jeshi la Syria, Bwana Erdogan aliiambia serikali kurejea katika mstari wa uangalizi la sivyo wakabiliane na mashambulio ya kijeshi.

Jumanne, msemaji wa rais wa Uturuki alisema katika mazungumzo baina ya wajumbe wa Uturuki na Urusi mjini Moscow bado hajapata "matokeo ya kuridhisha".

Pendekezo la Urusi la "kuchora upya eneo salama halikukubalika na lilikua "halikua swali " kwa Uturuki kupeleka wanajeshi wake katika vituo vya ukaguzi, Ibrahim Kalinalielezea.

No comments:

Post a Comment

Adbox