Katika Youtube, hadi saa 10:26 ulikuwa umetazamwa mara 425,178.
Beatz ambaye jina lake halisi ni Kasseem Dean aliandika ujumbe katika ukurasa wa Diamond wa Instagram, akimuomba amtumie wimbo huo, Diamond amekubaliana na ombi hilo.
Mtayarishaji huyo maarufu wa muziki ambaye ni mume wa msanii Alicia Keys ameshawatengenezea nyimbo wanamuziki maarufu nchini Marekani akiwemo Beyonce katika wimbo wa Check on It na Ring the Alarm.

No comments:
Post a Comment