Meli hiyo ´´MS Westerdam´´ iliyowabeba abiria 1,455 na wafanyakazi 802 imetia nanga kwenye mjini wa bandari wa Cambodia wa Sihanoukville jana Alhamisi.
Kabla ya kuruhusiwa kuingia bandarini maafisa wa Cambodia walitumwa ndani ya chombo hicho kuchukua vipimo vya abiria waliokuwa na dalili za mafua au afya dhaifu ya mwili.
Wizara ya afya ya Cambodia imesema baada ya vipimo hakuna mtu aliyebainika kuambukizwa virusi vya Corona na abiria wameruhusiwa kuanza kutemremka kutoka melini leo asubuhi.


No comments:
Post a Comment