Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi katika Shirikisho la Tanzania , TFF Malangwe Mchungahela amesema kutakuwa na uchaguzi mdogo katika Bodi ya Ligi (TPLB) utakaofanyika Desemba 7 mwaka huu ili kujaza nafasi sita zilizo wazi.
Nafasi zilizo wazi ni wajumbe watatu kutoka vilabu vya ligi kuu, wajumbe wawili kutoka vilabu vya ligi daraja la kwanza na mjumbe mmoja kutoka ligi daraja la pili.
Akizungumza na wanahabari Mchungahela amesema mchakato wa kutangaza nafasi za wagombea umeanza leo huku zoezi la kuchukua fomu likianza Oktoba 12 mpaka Oktoba 16.
Amesema mgombea ni lazima awe Mwenyekiti/Rais wa klabu ya ligi kuu, ligi daraja la kwanza na ligi daraja la pili.
Friday, October 11, 2019
Uchaguzi Mdogo Bodi ya Ligi kufanyika Desemba 7
Tags
# Top News
About Sultan Mapigo
SULTAN MAPIGO: Kuwa wa kwanza kuhabarika, Tafadhari usisahau kusubscribe kushare na kucomment
Top News
Tags:
Top News
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


No comments:
Post a Comment