Waziri wa Mambo ya Nje, Profesa Palamagamba Kabudi ametangaza leo kuwa serikali kwa kushirikiana na Barrick Gold Corporation wameunda kampuni ya ubia inayoitwa Twiga Mineral Corporation.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Dar es Salaam Waziri Kabudi amesema ‘sasa amezaliwa mtoto mpya baada ya Barrick kukubali kumuua mtoto wake, Acacia.’
Kwa mujibu wa Prof. Kabudi akizungumza na waandishi wa habari, katika kampuni hiyo serikali ina hisa asilimia 16 na Barrick asilimia 84.
“Twiga Minerals Company Limited itakuwa na makao makuu yake jijini Mwanza. Kampuni hii imeundwa baada ya kufutwa kwa Acacia iliyokuwa na makao makuu yake jijini London,” alisema Kabudi.
Sunday, October 20, 2019
Serikali na Barrick waunda kampuni mpya ya Madini
Tags
# Top News
About Sultan Mapigo
SULTAN MAPIGO: Kuwa wa kwanza kuhabarika, Tafadhari usisahau kusubscribe kushare na kucomment
Top News
Tags:
Top News
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment