Ikiwa Imesalia siku moja kabla ya kufungwa kwa zoezi la kuandikisha wananchi kwenye Daftari la kudumu la Wapiga kura kwajili ya Kuchagua viongozi wa ngazi ya Mtaa, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda kwa kutambua umuhimu wa zoezi hilo amewaelekeza wenye maduka kufungua maduka yao Kesho October 14 kuanzia saa tano ili kutoa nafasi kwa wananchi kwenda kujiandikisha.
RC Makonda amesema kwakuwa kesho ni Siku ya Kumbukumbu ya Miaka 20 ya kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ameona ni vyema Wananchi wote wakamuenzi Baba wa Taifa kwa kuhakikisha wanapata Nafasi ya Kutosha ya Kujiandikisha ili waweze kuchagua Viongozi wa mitaa wanaoweza kutatua matatizo yao.
Aidha RC Makonda amewasihi Wamachinga, Bodaboda, Makondakta, madereva, Viongozi wa Taasisi, wafanyakazi wa Bar, Saloon, wamiliki na wafanyakazi wa Sehemu za Starehe kuhakikisha wanajiandikisha kwenye Ofisi za Serikali ya Mtaa, Shule za Msingi, sekondari na sehemu zilizowekwa mahema maalumu ya kujiandikisha
Sunday, October 13, 2019
Home
/
Top News
/
RC Makonda aelekeza maduka yote Dar kufunguliwa kesho saa tano asubuhi ili kutoa nafasi kwa wananchi kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura
RC Makonda aelekeza maduka yote Dar kufunguliwa kesho saa tano asubuhi ili kutoa nafasi kwa wananchi kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura
Tags
# Top News
About Sultan Mapigo
SULTAN MAPIGO: Kuwa wa kwanza kuhabarika, Tafadhari usisahau kusubscribe kushare na kucomment
Top News
Tags:
Top News
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


No comments:
Post a Comment