Rais wa Mexico Andres Manuel Lopez Obrador, ametetea uamuzi wa kumuachilia huru mtoto wa mlanguzi wa kimataifa wa dawa za kulevya Joaquin "El Chapo" Guzman, aitwaye Ovidio Guzman.
Ovidio aliachiliwa baada ya vikosi vya usalama kuzidiwa nguvu na wafuasi wa mtandao wa El Chapo.
Rais Obrador amesema anatambua kuwa hali ilikuwa ngumu wakati polisi walipokabiliana kwa risasi na kundi hilo Alhamisi. Amesema, kukamatwa kwa mhalifu mmoja hakuna thamani zaidi ya maisha ya raia.
Awali, mkuu wa vikosi vya usalama Alfonso Durazo alisema maafisa wa jeshi la ulinzi walikuwa wakilinda doria kwenye eneo la Culiacan walipoanza kushambuliwa kutoka nyumba jirani.
Maafisa hao walijibu mashambulizi na kuwakamata watu wanne, akiwemo mtu aliyejitambulisha kama Ovidio Guzman Lopez.
Ovidio alishtakiwa nchini Marekani mnamo mwaka 2018 kwa kusambaza dawa za kulevya. Mahakama ya Marekani ilimhukumu baba yake Joaquin "El Chapo" Guzman kifungo cha maisha jela.
Saturday, October 19, 2019
Rais wa Andres Manuel Lopez Obrador atetea mtoto wa El Chapo kuachiliwa
Tags
# Top News
About Sultan Mapigo
SULTAN MAPIGO: Kuwa wa kwanza kuhabarika, Tafadhari usisahau kusubscribe kushare na kucomment
Top News
Tags:
Top News
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment