Rais Magufuli amewataka viongozi wa mikoa kuwahamasisha wananchi kujiandikisha kwa ajili ya kupiga kura katika uchaguzi wa Serikali za mitaa.
“Jana Waziri alitoa takwimu za baadhi ya mikoa iliyofanya vizuri. Ninafuatilia lakini alitoa baadhi ya mikoa inayoendelea kufanya vibaya. Zoezi likikamilika nitataka Waziri anipe taarifa za mikoa iliyofanya vizuri na iliyofanya vibaya.”
“Nataka niseme hapa hadharani, ile mikoa ambayo watu wao watashindwa kuwahamasisha wananchi kujiandikisha kupiga kura nitawashangaa. Ninajua Watanzania hawatanilaumu kwa hatua zitakazochukua,” amesema Magufuli.
Ametoa kauli hiyo siku moja baada ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Tamisemi), Selemani Jafo kuahidi kupeleka pendekezo maalum kwa mikoa itakayofanya vibaya katika uandikishaji wakati akitoa taarifa za zoezi hilo jana mkoani Katavi mbele ya kiongozi mkuu huyo wa nchi.
Saturday, October 12, 2019
Home
/
Top News
/
Rais Magufuli atoa neno kwa viongozi watakaoshindwa kuhamasisha uandikishaji Serikali za mitaa
Rais Magufuli atoa neno kwa viongozi watakaoshindwa kuhamasisha uandikishaji Serikali za mitaa
Tags
# Top News
About Sultan Mapigo
SULTAN MAPIGO: Kuwa wa kwanza kuhabarika, Tafadhari usisahau kusubscribe kushare na kucomment
Top News
Tags:
Top News
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


No comments:
Post a Comment