Mahujaji 35 wamefariki na wengine wanne kujeruhiwa katika ajali ya basi karibu na mji mtakatifu wa Saudia wa Madinah.
Ajali hiyo ilitokea Jumatano jioni wakati basi lililokuwa limebeba mahujaji 39 wa nchi tofauti za Asia na Kiarabu lilipogongana na gari lingine katika Kituo cha Al-Akhal eneo la Madinah.
Polisi wa Madinah wameanzisha uchunguzi ili kubaini kilichosababisha ajali hiyo.
Gavana wa Madinah Prince Faisal bin Salman bin Abdulaziz alituma ujumbe wa rambirambi kwa jamaa na marafiki wa waathirika na kuwatakia afueni ya haraka kwa waliojeruhiwa.
Thursday, October 17, 2019
Madinah: Mahujaji 35 wafariki katika ajali ya basi
Tags
# Top News
About Sultan Mapigo
SULTAN MAPIGO: Kuwa wa kwanza kuhabarika, Tafadhari usisahau kusubscribe kushare na kucomment
Top News
Tags:
Top News
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


No comments:
Post a Comment