Adelina Kapaya-Katavi
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi, John Lomuri ameunda kamati maalumu ya kushughurikia maandalizi ya kuhamisha ofisi zote za Wilaya ya Tanganyika kutoka katia wilaya ya Mpanda kuhamia ndani ya wilaya ya Tanganyika.
Hayo yamebainishwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mpanda, Samson Medda na kubainisha kuwa wako kwenye mkakati wa kuhakikisha wanahamia katika Halmashauri ya Tanganyika kutokana na agizo la Rais na ifikapo wiki ijayo Ofisi ya Mkurugenzi itahamia katika jengo la Hospitali ya Wilaya huku ujenzi ukiendelea.
Samson ameongezea kwa kusema kuwa licha ya ofisi zao kuwa mbali na Wilaya yao wamekua wakifanya kazi zao kwa uadilifu kwa kuwahudumia wananchi pamoja na kutatua changamoto zinazowakabili kwa muda mwafaka na kuyatafutia suluhu
Licha ya Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, John Magufuli kutoa agizo kwa wakurugenzi wote nchi nzima kuhakikisha wanahamia katika wilaya zao, wilaya ya Tanganyika ilikuwa imeshaanda maeneo ya kujenga ofisi za Halmashauri kwa lengo la kuihudumia jamii kwa ukaribu zaidi ili kupunguza gharama za usafiri wakati wa utendaji
Mnamo October 7 mwaka huu Rais Magufuli alimtaka Mkurugenzi Mtendaji wilaya ya Tanganyika kuhakikisha wanahamia katika Halmashauri yao na ofisi zao zote ziwe ndani ya wilaya husika kwa muda wa siku 30.
Monday, October 21, 2019
Kamati yaandaliwa kutekeleza agizo la Rais Magufuli
Tags
# Top News
About Sultan Mapigo
SULTAN MAPIGO: Kuwa wa kwanza kuhabarika, Tafadhari usisahau kusubscribe kushare na kucomment
Top News
Tags:
Top News
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment