Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa anatarajia kufanya Ziara ya siku nne ya Kikazi Mkoani Singida, kwaajili ya kukagua na kutembelea miradi ya Maendeleo ikiwemo ile mikubwa ya Kitaifa na kufungua rasmi maonyesho ya SIDO Kitaifa mjini Singida.
Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo Ofisini kwake Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk Rehema Nchimbi amesema ziara ya waziri itaanzia katika Wilaya ya Manyoni akitokea Mkoani Dodoma na kuhitimisha siku ya Jumatatu ya October 8 mwaka huu.
Naye Mkurugenzi mkuu wa SIDO Profesa Sylvester Mpandu amesema kuwa maonyesho ya mwaka huu yatakuwa na mvuto mkubwa kutokana na ushiriki wa mataifa Makubwa ikiwemo China,India na Afrika kusini ambayo yamepiga hatua kubwa kwa teknolojia ya Viwanda.
Monday, September 30, 2019
Waziri Mkuu kufungua Maonyesho ya Sido mkoani Singida
Tags
# Top News
About Sultan Mapigo
SULTAN MAPIGO: Kuwa wa kwanza kuhabarika, Tafadhari usisahau kusubscribe kushare na kucomment
Top News
Tags:
Top News
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


No comments:
Post a Comment