Adbox

Monday, September 2, 2019

Mwenge wa Uhuru wakataa mradi wa Madarasa

Na Rahel Nyabari, Tabora

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2019, Mzee Mkongea Ally amekataa kuzindua  mradi wa ujenzi wa madarasa mawili katika Shule ya Sekondari Chang'a iliyopo Kata ya Tumbi  Manispaa ya Tabora baada ya kutilia shaka matumizi ya fedha kiasi cha shilingi Milioni nne.


Katika mradi huo wananchi wamechangia kiasi cha shilingi milioni kumi, Serikali kuu shilingi  milioni ishirini na moja huku Halmashauri katika ripoti  hiyo ikionesha kuchangia kiasi cha  shilingi  milioni  tatu wakati  uhalisia ikielezwa ni shilingi milioni Saba, wasiwasi ukaibuka katika matumizi ya milioni nne ambayo hayakuonekana kwenye  ripoti ya utekelezaji .

Ally ameagiza Taasisi  ya kuzuia na kupambana na rushwa mkoa wa Tabora kufanya  uchunguzi  wa  kina na kutoa  majibu ndani ya wiki mbili ili kuweza kuchukua hatua kwa mtu yeyote atakaye husishwa sheli ichukuliwe zidi yake .

Hata hivyo Kiongozi huyo wa mbio za Mwenge wa Uhuru amemtaka mkuu wa wilaya ya Tabora  Komanya Erick Kitwala baada ya kufanyika kwa uchunguzi huo kuzindua na kuweka  jiwe  la  msingi  kwa niaba ya kiongozi huyo wa mbio za mwenge  wa uhuru kwa  mwaka 2019.

No comments:

Post a Comment

Adbox