Rais Magufuli ametoa Tsh. 500,000 kwa kila majeruhi wa ajali ya moto iliyotokea Morogoro jana alipowatembelea na kuwafariji katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Ameeleza hayo leo akiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alipokwenda kuwatembelea majeruhi wa ajali ya moto iliyotokea jana Msamvu Morogoro.
Pia Rais Magufuli pia ametoa motisha ya fedha kwa wauguzi na madaktari wanaotoa huduma kwa majeruhi hao.
“Serikali itagharamia gharama zote za matibabu kwa majeruhi, ninyi (madaktari) endeleeni kutoa huduma, na gharama zote mzilete serikalini, hawa wote ni Watanzania, tutawahudumia,” amesema.
Ameendelea kwa kusema, "Nasisitiza, tusiwe majaji, tusiwe wepesi kutoa hukumu, si kila aliyehusika katika ajali hii alikwenda kuchota mafuta, wengine walikuwa wanapita tu, wengine walikwenda kuokoa, wengine walikuwa na shughuli zao,”.
Sunday, August 11, 2019
Rais Magufuli atoa Tsh. 500,000 kwa kila Majeruhi wa ajali ya Moto Morogoro
Tags
# Top News
About Sultan Mapigo
SULTAN MAPIGO: Kuwa wa kwanza kuhabarika, Tafadhari usisahau kusubscribe kushare na kucomment
Top News
Tags:
Top News
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


No comments:
Post a Comment