Ni miaka 70 leo tangu kusainiwa kwa mikataba minne ya Geneva, iliyoweka msingi wa sheria ya kimataifa ya kulinda haki za binadamu. Lakini ingawa nchi 196 zimeitia saini mikataba hiyo, utekelezwaji wake unasuasua.Mikataba hiyo minne ya baada ya vita vikuu vya pili iliweka kanuni za kulinda haki za raia na wanajeshi katika mazingira ya vita. Ingawa nchi 196 ni wanachama wa mikataba hiyo, utekelezwaji wake wakati huu unakabiliwa na kitisho katika maeneo kadhaa ya mizozo.Kwa mujibu wa mikataba hiyo na itifaki kadhaa za nyongeza, raia na wanajeshi wanayo haki ya kutendewa ubinadamu katika mizozo ya kivita, na mashambulizi yoyote ya kijeshi yanaruhusiwa tu dhidi ya shabaha za kijeshi. Lakini, wakati mizozo ya kisasa ikijikita zaidi katika mazingira ya mjini, pande zinazohasimiana zimekuwa mara kwa mara zikiikiuka mikataba ya Geneva.
Monday, August 12, 2019
Mikataba ya Geneva yatimiza miaka 70
Tags
# Top News
About Sultan Mapigo
SULTAN MAPIGO: Kuwa wa kwanza kuhabarika, Tafadhari usisahau kusubscribe kushare na kucomment
Top News
Tags:
Top News
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


No comments:
Post a Comment