Serikali ya Tanzania kupitia jopo la Mawakili leo imewasilisha hoja nzito tatu za kisheria kupinga uamuzi wa awali wa Mahakama Kuu ya Gauteng, A. Kusini, kuizuia Ndege ya Tanzania, baada ya kusikiliza hoja hizo sasa Mahakama itatoa notisi ya siku ya kusomwa uamuzi wake.
Akizungumza kutoka Nchini Afrika Kusini Kiongozi wa ujumbe wa Tanzania Wakili Dkt. Damas Ndumbaro ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, amesema kwa hoja hizo tatu za kisheria anaamini Mahakama imeelewa kasoro za uamuzi wa awali na itatenda haki.
Kesho katika mkutano wangu na Wanahabari saa 4 asubuhi hapa Jijini Dodoma, nitaeleza kwa kina msingi wa kisheria wa hoja 3 ambazo Tanzania imeziwasilisha na ambazo tunaamini zitawarejeshea Watanzania haki yao.
Friday, August 30, 2019
Kauli ya Serikali kuhusu ndege iliyokamatwa Afrika Kusini
Tags
# Top News
About Sultan Mapigo
SULTAN MAPIGO: Kuwa wa kwanza kuhabarika, Tafadhari usisahau kusubscribe kushare na kucomment
Top News
Tags:
Top News
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


No comments:
Post a Comment