Sudan itasheherekea hii leo makubaliano ya kihistoria yaliyofikiwa kati ya majenerali wa kijeshi na viongozi wa waandamanaji, juu ya kuundwa kwa serikali ya kiraia, ambayo wengi wanatumai italeta mafanikio.
Katika sherehe hiyo itakayofanyika katika ukumbi mmoja mjini Khartoum, wanachama wa baraza la mpito la kijeshi na viongozi wa waandamanaji watatia saini nyaraka katika hafla hiyo.
Mpango huo uliofikiwa Agosti 4 unaashiria kumalizika kwa mgogoro wa kisiasa wa takriban miezi minane. Kabla ya hapo raia wengi wa Sudan waliandamana kupinga utawala wa Omar al Bashir ambaye hatimaye aliondolewa madarakani mwezi Aprili baada ya kuiongoza Sudan kwa miaka 30.
Muundo wa baraza kuu la mpito lenye wingi wa wajumbe wa kiraia litatangazwa rasmi hapo kesho Jumapili.
Saturday, August 17, 2019
Sudan kusherehekea makubaliano ya kihistoria
Tags
# Top News
About Sultan Mapigo
SULTAN MAPIGO: Kuwa wa kwanza kuhabarika, Tafadhari usisahau kusubscribe kushare na kucomment
Top News
Tags:
Top News
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


No comments:
Post a Comment